NEWS

Manara Amshutumu Karia kwa Ulevi wa Madaraka, Amshinikiza Aombe Radhi

Manara Amshutumu Karia kwa Ulevi wa Madaraka, Amshinikiza Aombe Radhi

Aliyekuwa msemaji wa klabu ya Yanga, Haji Manara, ametoa majibu makali kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, kufuatia kauli yake kuhusu uamuzi wa kuahirisha mchezo wa Kariakoo Derby uliopaswa kuchezwa Machi 8, 2025.

Katika majibu yake, Manara amemshutumu Karia kwa kile alichokiita “ulevi wa madaraka” na kusisitiza kuwa mechi hiyo haitachezwa hadi pale haki itakapotendeka. Aidha, amemtaka Rais huyo wa TFF kuomba radhi kwa kauli zake ambazo zimezua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka nchini.

About the author

Chanky Supplier